Tuesday, January 27, 2015

VAN PERSIE ADAI HAJUI HATMA YAKE UNITED.

MSHAMBULIAJI wa Manchester United Robin van Persie amekiri hajui kama atapewa ofa ya mkataba mpya wakati ule wa sasa utakapomalizika mwaka 2016. Akihojiwa nyota huyo wa wa kimataifa wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 31, amesema hilo sio suala lake kujua kwani anachofahamu kwasasa atakuwepo Old Trafford kwa miezi 18. Van Persie amesema baada ya kumaliza makataba wake hajui kitakaochoendelea baada ya hapo kwani anaweza kuwepo au kuondoka kwenda kwingine. Nyota huyo pia hadhani kama amefunga mabao ya kutosha toka kuanza kwa msimu huu hivyo amepania kuongeza bidii na kuhakikisha anafunga mabao mengi zaidi ili kuisadia timu yake. Van Persie mpaka sasa amefunga mabao nane katika mechi 21 za mashindano yote alizocheza msimu huu na kumaanisha kuwa itakuwa ngumu kufikia rekodi yake ya mabao 18 katika mechi 30 alizocheza katika msimu wake wa kwanza akitokea Arsenal mwaka 2012.

AFCON 2015: DRC, TUNISIA ZAUNGANA NA GUINEA YA IKWETA NA CONGO KATIKA ROBO.

JAMHURI ya Kidemokrasia ya Congo-DRC imekuwa timu pekee kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kusonga hatua ya robo fainali ya michuano Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Tunisia. DRC imesonga mbele wakiwa washindi wa pili wa kundi B nyuma ya Tunisia ambao wao nao wamepita kama vinara wa kundi hilo. Pamoja na DRC kumaliza wakiwa na alama sawa na Cape Verde idadi ya mabao ya kufungwa na kufunga ndio yaliyowavusha. Mabingwa wa michuano hiyo mwaka 2012 Zambia ambayo ndio timu nyingine inayotoka katika ukanda wa huu walishindwa kufurukuta mbele ya Cape Verde na kutoka sare ya bila kufungana hatua ambayo imewafanya kumaliza wakiburuza mkia wa kundi hilo. Leo kutakuwa na kinyang’anyiro kingine cha kugombea nafasi mbili za juu kutinga robo fainali katika kundi C ambapo Senegal watakuwa na kibarua kizito dhidi ya Algeria huku Afrika Kusini nao wakipepetana na Ghana. Kundi kama ilivyo mengine liko wazi ambao timu itakayoibuka na ushindi itakuwa imejiwekea nafasi nzuri yakusonga mbele.

Monday, January 26, 2015

RATIBA YA FA: ARSENAL WAPANGWA NA WABABE WA CITY, MAN UNITED KUENDELEA KUPETA KAMA WAKISHINDA MECHI YAO YA MARUDIANO DHIDI YA CAMBRIDGE.

MABINGWA watetezi Arsenal wamepangwa na timu ya daraja ya kwanza la Middlesbrough katika mzunguko wa tano wa michuano ya Kombe la FA. Middlesbrough ambao waliing’oa Manchester City katika mzunguko wa nne wataifuata Arsenal katika uwanja wao wa Emirates mwishoni mwa wiki ya Februari 14 na 15 mwaka huu. Bradford City waliopo ligi daraja la pili wao wamezawadiwa kwa kuitoa Chelsea kwa kupewa mchezo wa nyumbani dhidi ya aidha Sunderland au Fulham. Mshindi katika mchezo kati ya Cambridge United na Manchester United anatarajiwa kukutana na aidha Preston au Sheffield United. Katika michezo mingine ya mzunguko wa tano Crystal Palace wao watakuwa wenyeji wa mshindi kati ya Liverpool au Bolton Wanderers wakati Aston Villa watakwaana na Leicester City na West Bromwich Albion wao watachuana na West Ham United.

Saturday, January 24, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: JUVENTUS KUMUUZA POGBA KWA EURO MILIONI 100 KIANGAZI, CHELSEA YAONGEZA DAU KWA COSTA.

KATIKA habari za tetesi za usajili klabu ya Juventus imepanga kumuachia Paul Pogba kama watapewa ofa ya paundi milioni 100 katika kipindi cha majira ya kiangazi. Klabu za Manchester City, United na Chelsea zinamfukuzia nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa kama ilivyo kwa klabu za Paris Saint-Germain na Bayern Munich. Chelsea wameongeza ofa yao kufikia euro milioni 25 kwa ajili ya kumsajili Douglas Costa huku wakijipanga pia na kumsajili Juan Cuadrado wa Fiorentina. Nyota hao wa Amerika Kusini wanategemewa kutua Stamford Bridge kuja kuziba nafasi ya za Andre Schurrle na Mohamed Salah ambao wanatarajiwa kuondoka katika kipindi hiki cha usajili wa Januari. Manchester United wameamua kumvalia njuga beki wa kulia wa Southampton Nathaniel Clyne ambapo wamemua kumtengea ofa ya kitita cha euro milioni 27. Meneja wa Queens Park Rangers, Harry Redknapp anajipanga kumfukuzia mshambuliaji wa Monaco Dimitar Berbatov katika kipindi hiki cha usajili wa Januari. Nyota huyo alimuambia Redknapp kuwa anataka kurejea katika Ligi Kuu huku akidaiwa kuigharimu QPR euro milioni 1.3 kama wakimchukua. Klabu za Manchester United na Arsenal zinapigana vikumbo katika kumfukuzia nyota wa klabu ya Dinamo Moscow Aleksandar Dragovic ambapo meneja Arsene Wenger ameamua kutuma maskauti wake kumuangalia katika mchezo wa kirafiki. Wenger anamchukulia mchezaji huyo kama karata yake ya pili kama akishindwa kumsajili Gabriel Paulista.

Friday, January 23, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: CHELSEA YAKUBALI KUIPA FIORENTINA PAUNDI MILIONI 23 KWA AJILI YA CUADRADO, MAN UNITED YAMVIZIA ALVES KIANGAZI.

KATIKA habari tetesi za usajili, klabu ya Chelsea hatimaye imefikia makubaliano na klabu ya Fiorentina kwa ajili ya kumsajili Juan Cuadrado kwa kitita cha paundi milioni 23. Chelsea sasa wameruhusiwa kuzungumza na nyota huyo wa kimataifa wa Colombia mwenye umri wa miaka 26 kwa ajili ya makubaliano binafsi wakati wakijipanga kumuuza Mohamed Salah. Arsenal wameingia katika kinyang’anyiro cha kumuwania kiungo wa Roma Radja Nainggolan lakini wanakabilwia na kibarua kizito kutoka na klabu za Manchester United na Chelsea nazo kumuwinda kiungo huyo anayekadiriwa kuwa na thamani ya paundi milioni 26. Manchester United wanazidisha kupata uhakika wa kumsajili Dani Alves kutoka Barcelona kwa uhamisho huru katika majira ya kiangazi. Kocha wa United Louis van Gaal amepania kumsajili beki huyo wa kulia na anamatumaini Victor Valdes anaweza kumshawishi mchezaji mwenzake wa zamani kuhamia Old Trafford. Kiungo Yann M’Vila amerejea katika klabu yake ya Rubin Kazan baada ya Inter Milan kuamua kutengua mkpo wa mchezaji huyo kufuatia kuonyesha kiwango kibovu. Liverpool nao wanajipanga kutoa ofa kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Southampton Jay Rodriguez kabla ya dirisha la usajili wa Januari halijafungwa. Winga huyo wa kimataifa wa Uingereza anatarajiwa kurejea uwanjani baada ya kupona majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua wiki hii. Manchester United wanajipanga kufanya usajili wa wachezaji watatu wakubwa katika majira ya kiangazi ambapo kocha Louis Van Gaal amepanga kuwasajili kiungo wa Roma Kevin Strootman, beki wa Borussia Dortmund Mats Hummels na beki wa kulia wa Southampton Nathaniel Clyne.

MADRID YAMNASA LUCAS SILVA.

MAKAMU rais wa klabu ya Cruzeiro Marcio Rodriguez amedai kuwa uhamisho wa Lucas Silva kwenda Real Madrid umeshafikia hatua nzuri ya makubaliano. Kwa kipindi kirefu Madrid iliyo chini Carlo Ancelotti imekuwa ikimfukuzia kiungo huyo chipukizi mwenye umri wa miaka 21. Rodriguez amesema uhamisho wa Silva tayari umekamilika na kilichokuwa kikisubiriwa ni Madrid wenyewe kutangaza rasmi. Rodriguez aliendelea kudai kuwa hawata pata tabu kutafuta mbadala wake kwani kuna wachezaji wengi ambao wako tayari kupandishwa.

TER STEGEN AAPA KUPIGANIA NAMBA BARCELONA.

GOLIKIPA wa kimataifa wa Ujerumani Marc-Andre Ter Stegen amekiri kuwa hana furaha katika nafasi yake kama gilikipa namba mbili na amejipanga kuhakikisha anakuwa kinara wa klabu ya Barcelona. Golikipa huyo mwenye umri wa miaka 22 alijiunga na Barcelona akitokea Borussia Monchengladbach Mei mwaka jana lakini kocha Luis Enruque anamtegemea zaidi Claudio Bravo kama kipa namba moja. Hata hivyo, Ter Stegen bado anamatumaini kuwa ataweza kumzidi uwezo golikpa huyo wa kimataifa wa Chile wakati wowote katika msimu huu unaondelea. Akihojiwa Ter Stegen amesema anafurahia anavyoungwa na mkono na mashabiki na kazi anayofanya na wachezaji wenzake lakini hafurahishwi na kuwa kwake chaguo la pili.