OFISA mkuu wa zamani wa Chama cha Soka nchini Uingereza-FA, Mark Palios amesema ameshangazwa na kauli ya Sol Campbel aliyedai kuwa hakuchaguliwa kuwa nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza kwasababu ya rangi yake. Campbell mwenye umri wa miaka 39 anaamini kuwa angeweza kuwa nahodha wa nchi hiyo kwa miaka 10 kama angekuwa mweupe. Akihojiwa Campbell ambaye ameichezea Uingereza mechi 73 amesema anadhani FA walikuwa wakitamani awe mzungu. Palios ambaye aliiongoza FA mwaka 2003-2004 amesema kauli hiyo imemshangaza kwasababu sio jukumu la FA kuteua manahodha wa timu ya taifa bali jukumu hilo analo kocha. Campbell ambaye amewahi kuwa beki wa Arsenal na Tottenham huku akiichezea Uingereza kuanzia mwaka 1996 hadi 2007 aliwahi kuwa nahodha wan chi hiyo mara tatu wakati timu ikiwa chini ya Sven Goran Eriksson.
No comments:
Post a Comment