Friday, January 13, 2012

GERRARD AJIPIGA KITANZI CHA MUDA MREFU NA LIVERPOOL.

Nahodha wa klabu ya Liverpool Steven Gerrard amethibitisha kuwa amesaini mkataba mpya na mrefu na klabu hiyo ambao utamuweka hapo mpaka hapo atakapotundika daruga. Hatahivyo sio klabu hiyo wala Gerrard mwenyewe aliyesema mkataba huo utakuwa ni wa muda gani. Kiungo huyo wa kimataifa wa Uingereza ambaye alianza kuichezea klabu hiyo akiwa na miaka 18 Novemba mwaka 1998 ameshacheza mechi 566 na klabu hiyo na ameshinda mabao 144 likiwemo la penati alilofunga Jumatano dhidi ya Manchester City katika nusu fainali ya kwanza ya Kombe la Ligi. Mchezaji huyo pia ameichezea timu ya taifa ya Uingereza mara 89 na kushinda mabao 19. Gerrard ameisaidia klabu hiyo kushinda vikombe viwili FA pamoja na Kombe la Ligi mara mbili na kimoja cha Klabu Bingwa ya Ulaya lakini mchezaji huyo anasikitika kutokushinda kombe la Ligi Kuu ya nchi hiyo katika kipindi chote ambacho ameichezea klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment