
Monday, August 20, 2012
FEDERER ANYAKUWA TAJI LA CINCINNATI.
MCHEZA tenisi nyota kutoka Switzerland, Roger Federer amefanikiwa kumfunga Novak Djokovic wa Serbia katika mchezo wa fainali ya michuano ya wazi ya Cincinnati na kufanikiwa kunyakuwa taji hilo kwa mara ya tano. Federer ambaye ni bingwa wa michuano ya Wimbledon alimfunga Djokovic kwa 6-0 7-6 9-7 na kufanikiwa kunyakuwa taji hilo. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Federer amesema kuwa amefurahi kushinda taji hilo na anajiona yuko katika kiwango bora kwa ajili ya michuano ya wazi ya Marekani inayotarajiwa kuanza Agosti 27 mwaka huu jijini New York. Federer mwenye umri wa miaka 31 ambaye alifungwa na Andy Murray katika michuano ya Olimpiki, sasa anakuwa ameshinda mataji sita ya ATP kwa mwaka huu. Kwa upande wa wanawake Li Na wa China alifanikiwa kunyakuwa taji hilo kwa kumfunga Angelique Kerber wa ujerumani kwa 1-6 6-3 6-1 likiwa ni taji lake la sita la michuano ya WTA.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment