Wednesday, February 19, 2014

KWELI NILIKOSEA LAKINI SIKUFANYA NGONO - GIROUD.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Arsenal, Olivier Giroud amejaribu kuweka wazi juu ya maisha yake binafsi kwa kusisitiza kuwa hakufanya uzinzi kama watu wanavyofikiria. Nyota huyo aliomba radhi baada ya picha yake iliyopigwa na mwanamitindo Celia Kay katika hoteli ya Four Seasons ambayo Arsenal walifikia kabla ya mchezo wao dhidi ya Crystal Palace uliochezwa Februari 2 kuonekana gazetini. Giroud aliandika tena katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuwa aliomba msamaha na kukiri kuwa alifanya kosa lakini hakufanya ngono na mwanamitindo huyo. Wenger alithibitisha kumchukulia hatua mchezaji huyo kwa tukio hilo lakini alikataa kuweka wazi adhabu atakayopewa kwa kudai kuwa ana heshimu mambo binafsi ya mchezaji huyo. Kulikuwa na tetesi kuwa Arsenal walikuwa wamepanga kumpa adhabu ya faini ya paundi 230,000 kwa tukio hilo lakini walisitisha baada ya mchezaji huyo kukana huku wakili wake akituma barua kuelezea kuwa mteja wake hakufanya chochote kibaya.

No comments:

Post a Comment