Tuesday, July 1, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: KLINSMANN AIKOSOA FIFA KWA KUMTEUA MWAMUZI WA ALGERIA KUCHEZESHA MECHI YAO.

KOCHA wa timu ya taifa ya Marekani, Jurgen Klinsmann amelikosoa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa kumteua mwamuzi wa Algeria kuchezesha mchezo wao wa hatua ya mtoano wa Kombe la Dunia dhidi ya Ubelgiji baadae leo. Marekani walifunga bao la ushindi katika dakika za majeruhi kwenye michuano hiyo miaka minne iliyopita na kuwafanya kuongoza kundi lao mbele ya Uingereza na Klinsmann amesema uteuzi wa mwamuzi huyo Djamel Haumoudi hajaridhika nao. Klinsmann amesema hajaridhika na uamuzi huo kutokana na ukweli kuwa waliifunga Algeria katika michuano ya Kombe la Dunia iliyopita. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa anajua mwamuzi huyo amechezesha mechi mbili zilizopita vizuri hivyo ni mategemeo yake na mchezo huo ataumudu vyema.

No comments:

Post a Comment