Tuesday, July 1, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: NEYMAR FITI KUIKABILI COLOMBIA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Brazil, Neymar anategemewa kuwa fiti kwa ajili ya mchezo wa robo fainali ya michuano ya Kombe la Dunia dhidi ya Colombia utakaochezwa Ijumaa hii. Neymar mwenye umri wa miaka 22, alipata majeruhi ya paja la mguu wa kushoto na goti lake la kulia katika mchezo wa mtoano dhidi ya Chile ambao walishinda kwa changamoto ya mikwaju ya penati. Ofisa habari wa Shirikisho la Soka la Brazil, Rodrigo Paiva amesema majeruhi ya goti la Neymar ndio yaliyokuwa yakihofiwa sana lakini daktari wa timu Jose Luiz Runco amedai mashabiki hawapaswi kuwa na hofu kwani atakuwa fiti kwa ajili ya mchezo unaofuata. Paiva aliongeza kuwa Neymar anaweza kupumzishwa kufanya mazoezi kama itahitajika ikiwa ni juhudi za kumuweka fiti kabla ya mchezo wa Ijumaa.

No comments:

Post a Comment