Thursday, January 12, 2012
INTERPOL KUWASHUGHULIKIA WATAKAOUZA MECHI UEFA 2012.
SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA na Polisi wa Kimataifa-Interpol wanaungana kwa pamoja kupambana na tabia za upangaji wa matokeo pamoja na vurugu zinazoweza kutokea uwanjani. Interpol wamekubaliana kufanya kazi pamoja na UEFA kwa kupeleka askari wake katika michuano ya Ulaya itakayofanyika Poland na Ukraine baadae mwaka huu. Rais wa UEFA Michel Platin alithibitisha kukutana na Katibu Mkuu wa Interpol Ronald Noble Jumatano na wanatarajia kusaini mkataba wa makubaliano hayo mapema. Interpol tayari imejitolea kusaidia vyama vya soka na suala la upangaji wa matokeo ambapo wameshasaini makubaliano ya miaka 10 na Shirikisho la Soka la Dunia mwaka uliopita kufungua kituo nchini Singapore kuwafundisha wachezaji pamoja na waamuzi kuepuka rushwa katika michezo.
No comments:
Post a Comment