Wednesday, March 5, 2014

BARCELONA KUMFANYA MESSI KUWA MCHEZAJI ANAYELIPWA ZAIDI DUNIANI MWISHONI MWA MSIMU.

RAIS wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu amebainisha kuwa Lionel Messi atasaini na kuboresha mkataba mpya mwishoni mwa msimu huu ambao utamfanya kuwa mchezaji anayelipwa vizuri duniani. Klabu hiyo katika siku za karibuni ilidai kuwa inataka kumtunza nyota huyo wa kimataifa wa Argentina kwa ubora wake na sasa wameweka wazi nia yao ya kutaka kumfanya mchezaji huyo amalizie soka lake hapo. Bartomeu amesema nia ya klabu hiyo ni kutaka kumfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani na majira ya kiangazi jambo hilo litakamilika. Rais huyo amesema kuwa hawana mpango wa kumuuza nyota huyo wako naye na ni mategemeo yao atastaafu soka akiwa Camp Nou.

No comments:

Post a Comment