Monday, March 3, 2014

EL HADARY ATAMANI KUCHEZA KOMBE LA DUNIA 2018.

GOLIKIPA mkongwe wa kimataifa wa Misri, Essam El Hadary amedai kuwa anategemea kucheza michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Urusi mwaka 2018. El Hadary alirejea katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo baada ya kukosekana kwa mwaka mmoja kwa kushindwa kuelewana na kocha wa zamani Bob Bradley. Akihojiwa El Hadary amesema ndoto zake ni kucheza michuano hiyo ya Urusi na hajali umri wake kwasababu anajua atafanya vyema akienda huko. Kipa huyo anayejulikana nchini humo kwa jina la utani la High Dam alizaliwa mwaka 1973 huko Damietta na sasa anakipiga katika klabu ya Ligi Kuu ya Wadi Degla. El Hadary mwenye umri wa miaka 41 hivi sasa aliendelea kudai kuwa amecheza soka toka mwaka 1993 na anajua kama ukicheza kwa juhudi basi lazima utapata nafasi.

No comments:

Post a Comment