Tuesday, July 1, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: CAMEROON KUFANYIWA UCHUNGUZI TUHUMA ZA UPANGAJI MATOKEO.

MAOFISA wa Cameroon wanafanyia uchunguzi madai kuwa wachezaji wake saba walihusika na suala la upangaji matokeo katika michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Brazil. Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la Soka la Cameroon-Fecafoot inafanyia kazi tuhuma hizo za upangaji matokeo katika mechi tatu za hatua ya makundi walizocheza. Tuhuma hizo zimetolewa na gazeti moja la Ujerumani na Fecafoot wamenuia kuzifanyia kazi na kama ikigundulika kuna ukweli wahusika wote watachuliwa hatua stahiki. Cameroon alitandikwa katika mechi zao zote tatu katika kundi A, kikiwemo kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa Croatia.

No comments:

Post a Comment