Thursday, January 1, 2015

TETESI ZA USAJILI: MESSI AMTAKA LAVEZZI, MOURINHO KUMFUATA REUS DORTMUND.

WAKATI dirisha dogo la usajili likiwa limefunguliwa rasmi leo kumekuwa na taarifa na tetesi mbalimbali za usajili zinazoendelea kila pembe barani Ulaya. Tukianzia nchini Hispania kumekuwa taarifa zinazodai kuwa mshambuliaji nyota wa Barcelona Lionel Messi ameiomba timu hiyo kumsajili Ezequiel Lavezzi kutoka klabu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa. Taarifa hizo zimeendelea kudai kuwa Messi anataka kucheza pamoja na mshambuliaji mwenzake huyo kutoka Argentina. Tukisogea nchini Uingereza nako kuna tetesi kuwa meneja wa Chelsea Jose Mourinho amemuomba bosi wake Roman Abromovic kumsajili nyota wa kimataifa wa Ujerumani Marco Reus kutoka klabu ya Borussia Dortmund. Tukibakia hukohuko Uingereza, Arsenal nao wameibuka baada ya kudaiwa kuwa wanamuwinda kuingo wa Atletico Madrid Mario Suarez wakati kocha wa timu hiyo Arsene Wenger akijaribu kuimarisha kikosi chake. Tukirejea nchini Hispania kuna taarifa kuwa kampuni ya vifaa vya michezo kutoka Marekani ya Ander Armour inadaiwa kuanza mazungumzo na klabu ya Barcelona kwa ajili ya udhamini wa jezi zao hivyo kuzusha tetesi kuwa mkataba baina yake na kampuni ya Nike unaweza kusitishwa wakati wowote.

No comments:

Post a Comment