Thursday, January 1, 2015

BORO YAKUBALIANA NA CHELSEA KUENDELEA KUMTUMIA BAMFORD.

KLABU ya Middlesbrough imethibitisha kuongeza makubaliano ya mkopo na klabu ya Chelsea kwa ajili ya mshambuliaji Patrick Bamford mpaka mwishoni mwa msimu huu. Bamford amekuwa akionyesha kiwango kizuri toka ajiunge na Boro kwa mkopo wakati wa majira ya kiangazi mwaka jana akifunga mabao nane katika mechi 19 alizoichezea timu hiyo ambayo inashika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Daraja la Kwanza. Mkataba wake wa awali ulikuwa umalizike januari hii lakini Middlebrough wameamua kuongeza mkopo wa mshambuliaji mwenye umri wa miaka 21 ili aweze kuwasaidia katika kampeni zao za kurejea Ligi Kuu. Meneja wa timu hiyo Aitor Karanka amedai kuwa bamford anafurahia kuwepo hapo kwani anajifunza na kuimarika jambo ambalo ni muhimu kwa malengo yake pamoja na klabu. Bamford tayari ameshacheza kwa mkopo katika klabu za MK Dons na Derby County toka asajiliwe na Chelsea akitokea Nottingham Forest januari mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment