Tuesday, June 2, 2015

HATIMAYE BLATTER AAMUA KUACHIA NGAZI FIFA.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter ametangaza kujiuzulu wadhifa wake huo na kuitisha mkutano mkuu wa dharura ambao utafanyika uchaguzi wa kutafuta mbadala wake.Blatter mwenye umri wa miaka 79, alitangaza uamuzi wake huo mbele ya wana habari leo baada ya Katibu Mkuu wake Jerome Valcke mapema kuhusishwa na tuhuma za kuidhinisha dola milioni 10 kwenda kwa makamu wa zamani wa FIFA Jack Warner.Akitangaza uamuzi wake huo Blatter amesema amefikiria kwa makini kuhusu urais wake na miaka 40 ambao amekuwa ndani ya Shirikisho hilo na kwa mapenzi makubwa aliyonayo kwa mchezo wa soka ameamua kuachia ngazi.Blatter aliendelea kudai kuwa kingine kilichomsukuma kuachia ngazi ni kuona watu wengi hawadhani kama anaweza kulipeleka shirikisho hilo mbele jambo ambalo anaona lingerudisha nyuma mchezo wa soka kama angendelea kukaa madarakani.Uchaguzi kwa ajili ya kuziba nafasi ya Blatter unatarajiwa kupangwa kufanyika kati ya Desemba mwaka huu ay Machi mwakani.

No comments:

Post a Comment