Tuesday, August 16, 2016

HATIMAYE MARCOS REUS APATA LESENI.

WINGA wa kimataifa wa Ujerumani, Marco Reus ambaye alipigwa faini ya euro nusu milioni mwaka 2014 baada ya kugundulika kuendesha gari miaka kadhaa bila kuwa na leseni hatimaye amefanikiwa kufaulu majaribio ya udereva. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27, hakushiriki michuano ya Ulaya mwaka huu ambapo Ujerumani ilitolewa katika hatua ya nusu fainali na Ufaransa kutokana na majeruhi, hivyo aliutumia muda huo kujifunza sheria za barabarani na kujiandaa na jaribio la nadharia. Akihojiwa kuhusiana na hilo, Reus alithibitisha kuwa ni kweli amefaulu majaribio na kueleza furaha yake kuwa sasa suala hilo limepita salama. Reus ambaye ameicheza Ujerumani mechi 29, alifaulu majaribio ya nadharia na vitendo jana na alikabidhiwa leseni yake wakati akielekea mazoezini mapema leo.

No comments:

Post a Comment