Sunday, March 4, 2012
BRAZIL YAGOMA KUFANYA KAZI NA KATIBU MKUU WA FIFA.
Waziri wa Michezo wa Brazil Aldo Rebelo ametangaza kuwa serikali yake haitaki kushirikiana na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Jerome Valcke, baada ya malalamiko yake, ambayo amesema hayakubaliki. Kauli hiyo imekuja baada ya Valcke kulalamika juu ya matayarisho ya Brazili ya Kombe la Dunia la mwaka 2014. Rebelo amesema hayo baada ya Valcke kusema kwamba Brazil inaonesha kushughulishwa zaidi na kushinda Kombe la Dunia na kushindwa kuitayarisha nchi hiyo kwa ajili mashindano hayo. Valcke aliendelea kusema kuwa ujenzi wa viwanja vya michezo, miundo mbinu ya usafiri na mahoteli kwa ajili ya washabiki, umezorota hivyo nchi hiyo inahitaji kuzinduka ili kuharakisha shughuli hizo. Rebelo amesema kauli ya Valcke inakera na hailingani na tathmini njema iliyotolewa awali na shirikisho hilo wakati walipokuja kukagua maendeleo ya ujenzi huo. Waziri huyo aliongeza kusema kuwa serikali yake itaendelea kushirikiana na FIFA lakini siyo na Bwana Valcke
No comments:
Post a Comment