Sunday, March 4, 2012

MOURINHO AHOMA KUONGELEA SAFARI YAKE YA UINGEREZA.

MENEJA wa Real Madrid Jose Mourinho amekataa kuongelea mustakabali wake na klabu hiyo huko mbele baada ya kuonekana jijini London katikati ya wiki hii. Kuonekana kwa kocha huyo raia wa Ureno jijini London Jumanne wiki iliyopita kulizua chokochoko kuwa yuko tayari kurejea nchini humo mwishoni mwa msimu huu lakini wakati akihojiwa kabla ya mchezo dhidi ya Espanyol utakaochezwa jioni Mourinho hakutana kuzungumzia lolote kuhusu hilo. Mourinho amesema kuwa kabla ya kwenda huko aliomba ruhusa kwa Mwenyekiti wa klabu hiyo hivyo hahitaji kufafanua lolote kuhusu maisha yake binafsi kwa mtu mwingine yoyote zaidi ya waajiri wake. Madrid ndio inayoongoza Ligi Kuu nchini Hispania kwa tofauti ya pointi 10 na wapinzani wao wakubwa ambao ni mabingwa watetezi wa ligi hiyo klabu ya Barcelona.

No comments:

Post a Comment