Monday, April 1, 2013
CHAMPIONS LEAGUE: NI BARCA VS PSG, BAYERN VS JUVENTUS.
LIGI ya Mabingwa Ulaya hatua ya robo fainali inatarajiwa kuanza kutimua vumbi tena leo wakati timu nne zitakapojitupa dimbani katika mechi zao za kwanza za kutafuta tiketi ya kucheza nusu fainali ya michuano hiyo. Katika mchezo wa kwanza Barcelona wakiongozwa na nyota wake Andres Iniesta na Lionel Messi tayari wamewasili jijini Paris, Ufaransa kuikabili Paris Saint Germain ambao wanajivunia nyota wao Zlatan Ibrahimovic na David Beckham ambao imewasajili hivi karibuni. Mbali na mchezo huo pia kutakuwa na mchezo mwingine wa kukata na shoka kati ya vinara wa Ligi Kuu nchini Ujerumani timu ya Bayern Munich ambao watakuwa wenyeji wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu nchini Italia, Juventus katika Uwanja wa Alianz Arena. Juventus watakuwa na kibarua kizito kuidhibiti safu ya ushambuliaji ya Bayern ambayo imeonyesha kuwa katika kiwango cha juu baada ya kuibugiza Hamburger SV kwa mabao 9-2 katika mchezo wa ligi.
No comments:
Post a Comment