Monday, March 2, 2015

FEYENOORD YAANZA MAWINDO YA KOCHA MPYA.

KLABU ya Feyenoord inatarajia kuanza kutafuta kocha mpya baada ya Fred Rutten kutangaza kuwa anataka kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu. Rutten mwenye umri wa miaka 52 alichukua mikoba ya kuinoa ya timu hiyo kutoka kwa Ronald Koeman na kupewa mkataba wa mwaka mmoja kiangazi mwaka jana. Hata hivyo, kocha huyo amekuwa na akitofautiana na uongozi wa Feyenoord kuhusiana na mipango ya maendeleo. Akihojiwa Rutten amesema wote wamekuwa na malengo sawa lakini linafika suala la utekelezaji ili waweze kusonga mbele ndipo wanapotofautiana ndio maana ameamua kuachia ngazi mwishoni msimu.

No comments:

Post a Comment