Monday, March 2, 2015

MEIER AMGWAYA ROBBEN KATIKA MBIO ZA KUGOMBEA KIATU CHA DHAHABU BUNDESLIGA.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Eintracht Frankfurt, Alexander Meier hana shaka kuwa mshambuliaji wa Bayern Munich Arjen Rooben atakuja kuwa mfungaji bora wa Bundesliga msimu huu. Nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi kwasasa ndio anaongoza orodha ya wafungaji akiwa na mabao 17 katika mechi 19 alizocheza lakini Meier anamfuata kwa karibu akiwa nyuma yake kwa tofauti ya bao moja. Hata hivyo, Meier hadhani kama anaweza kupambana dhidi ya mshambuliaji huyo na ana hofu anaweza kubakia katika nafasi hiyohiyo ya pili. Nyota huyo amesema itakuwa ngumu kumshika Robben kwasababu katika mchezo mmoja ana uwezo wa kufunga bao moja au mawili. Robben na Meier ndio wachezaji pekee walioko katika mbio za kugombea taji la mfungaji bora wa Bundesliga msimu huu.

No comments:

Post a Comment