Monday, March 2, 2015

MALI MABINGWA WAPYA WA AFRIKA KWA VIJANA CHINI YA UMRI WA MIAKA 17.

MALI wametawadhwa mabingwa wapya wa michuano ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 baada ya kufanikiwa kuichapa Afrika Kusini kwa mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika huko Niemey Jumapili hii. Mabao ya kipindi cha pili yaliyofungwa na Siaka Bagayoko na Aly Malle yalitosha kuihakikishia Mali ushindi muhimu. Hiyo ni mara ya kwanza katika historia kwa Mali kunyakuwa taji hilo la mashindano ya vijana. Mara ya mwisho Mali kukaribia kunyakuwa taji hilo ilikuwa ni mwaka 1997 wakati walipomaliza kama washindi baada ya kufungwa na Botswana. Kwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo, Mali, Afrika Kusini, Guinea na Nigeria wote wamefuzu michuano ya Kombe la Dunia kwa vijana wa umri huo ambayo itafanyika nchini Chile Octoba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment