GOLIKIPA wa Tottenham Hotspurs Hugo Lloris amethibitisha kuwa hakuna kiwango chochote cha ada kilichowekwa kwake na klabu hiyo kufuatia taarifa kuwa Manchester United inahitaji kumsajili.Kulikuwa na taarifa kutoka Ufaransa zilizodai kuwa golikipa huyo mwenye umri wa miaka 28 alikuwa amewekewa kiwango cha euro milioni 20 kwa timu itakayomuhitaji kama Spurs wakishindwa kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.Lloris amebainisha kuwa anafanya mawasiliano ya karibu na mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy na kusisitiza kuwa atapewa taarifa kama kuna ofa yeyote itakayotolewa kwake majira haya ya kiangazi.Akiulizwa kuhusiana na kiwango hicho kilichowekwa, Lloris amesema katika mkataba wake hakuna kipengele kama hicho.Golikipa huyo aliendelea kudai kuwa kama ikitoka ofa nzuri ambayo itaziridhisha pande zote mbili anadhani anaweza kuondoka lakini kwasasa bado ataendelea kuwepo hapo kwani amekuwa na mahusiano mazuri na viongozi.
No comments:
Post a Comment