Tuesday, June 2, 2015

NI NGUMU KUZIKATALIA BARCELONA AU REAL MADRID.

MSHAMBULIAJI nyota wa Lyon, Alexandre Lacazette amesisitiza kuwa hajapata uamuzi juu ya mustakabali wake lakini amekiri kuwa itamuwia vigumu kukataa kwenda katika timu kama Barcelona au Real Madrid.Lacazette mwenye umri wa miaka 24 ndio mfungaji anayeongoza katika Ligi Kuu ya Ufaransa msimu huu, aliwa ameifungia Lyon mabao 27 na kuifanya kumaliza katika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi.Kutoka na hilo nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa amekuwa akihusishwa na tetesi za kutakiwa na vilabu kadhaa lakini mwenyewe amesema anataka kupumzika na kumuachia wakala wake kuzungumza na timu zinazomuhitaji.Akihojiwa Lacazette amesema hajaamua lolote mpaka sasa kwani anaenda zake likizo na kumuachia wakala wake masuala yote.

No comments:

Post a Comment