Friday, December 18, 2015

RAIS WA MADRID AMKANA MOURINHO.

RAIS wa Real Madrid, Florentino Perez amedai klabu hiyo haina mpango wa kumrejesha Jose Mourinho. Mourinho mwenye umri wa miaka 52, alishinda taji la La Liga na Kombe la Mfalme katika kipindi chake alipokuwa Bernabeu mwaka 2010 mpaka 2013 lakini jana alitimuliwa na Chelsea. Meneja wa Madrid Rafa Benitez yuko chini ya shinikizo kufuatia matokeo yasiyoridhisha msimu huu kikiwemo kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa mahasimu wao Barcelona. Akihojiwa Perez amesema hakuna anayejua mambo yajayo lakini kwasasa Mourinho hawezi kurejea Madrid.

No comments:

Post a Comment