Thursday, January 19, 2012

MWENYEKITI WA ARSENAL ADAI KLABU HIYO HAIWEZI KUYUMBA HATA KAM ITASHINDWA KUSHIRIKI CHAMPIONS LEAGUE.

MWENYEKITI wa klabu Arsenal Peter Hill-Wood amedai kuwa klabu hiyo haitakuwa katika hali mbaya kama itakosa tiketi ya kushiriki michuano ya KJlabu Bingwa ya Ulaya msimu huu. Arsenal inayonolewa na na kocha Arsene Wenger kwasasa inashika nafasi ya tano katika msimamowa Ligi Kuu nchini Uingereza wakiwa na alama nne nyuma ya Chelsea inayoshika nafasi ya nne huku Newcastle wakiwa nafasi ya sita na alama sawa na timu hiyo inayotoka Kaskazini mwa jiji la London. Kata hivyo Hill-Wood akiri kuwa itakuwa vizuri kama timu hiyo itamaliza msimu wa ligi hiyo ikiwa nafasi nne za juu amesema klabu hiyo siku zote huwa inajiandaa na hatima ya kutoshiriki michuano mikubwa ya vilabu barani Ulaya. Alipoulizwa kuhusu matumaini ya klabu hiyo kunyakuwa Kombe la Klabu Bingwa la Ulaya, Hill-Wood amesema bado wanapambana na hakuna la zaidi.

No comments:

Post a Comment