Wednesday, January 25, 2012

WAKALA WA BALOTELLI AMSHUTUMU MWAMUZI.

WAKALA wa mshambuliaji wa Manchester City Mario Balotelli amemshutumu mwamuzi Howard Webb kwa kudanganya kuwa mteja wake huyo alimpiga kichwa Luke Parker wa Tottenham Hotspurs wakati timu hizo zilipokutana Jumapili. Webb ambaye alikuwa mwamuzi katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010 hakuchukua hatua yoyote tukio hilo lilipotokea lakini alipohojiwa amesema kuwa kama angeliona hilo tukio basi lazima angempa kadi nyekundu Balotelli. Wakala huyo wa Balotelli anayeitwa Mino Raiola amesema amekasirishwa na kauli ya Webb akidai hakuliona tukio wakati wa mchezo huo wakati anaonekana hakuwa mbali na sehemu tukio lilipotokea wakati wa mchezo huo. Baada ya mchezo huo Shrikisho la Soka Uingereza-FA limetoa adhabu ya kumfungia michezo minne mchezaji huyo huku likimpa siku mbili kukata rufani.

No comments:

Post a Comment