Friday, March 2, 2012

FIFA KUFUATILIA USHAHIDI WA WARNER JUU YA FEDHA ZA HAITI.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA linafuatilia ushahidi aliowasilisha makamu wa rais wa zamani wa shirikisho hilo Jack Warner kuhusu upotevu wa fedha za msaada za Haiti baada ya tetemeko la ardhi lilitokea nchini humo 2010. FIFA imesema kuwa Warner amewasilisha maelezo yanayoeleza kwa undani kuhusu fedha hizo za msaada kiasi cha dola 250,000 alizoziomba na kupewa kwa ajili ya mradi wa kukuza soka katika nchi za Caribbean. Maofisa wa soka wa Haiti mwezi uliopita wakihojiwa na gazeti moja nchini Uingereza wamesema kuwa wamepokea kiasi cha dola 60,000 pekee kutoka kwa Warner. Wiki iliyopita Shirikisho la Soka la Trinidad na Tobago wamesema kuwa wanapanga kumshitaki Warner ili kuangalia uwezekano kurudisha mamilioni ya dola ambayo yamepotea kinyemela.

No comments:

Post a Comment