Tuesday, July 31, 2012

OLIMPIKI 2012: YE SHIWEN AKANA KUTUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU.

Ye Shiwen.
MUOGELEAJI kutoka China aliyeshinda medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki, Ye Shiwen amekanusha taarifa kuwa alikuwa ametumia madawa ya kuongeza nguvu katika mashindano hayo. Kocha wa timu ya waogeleaji kutoka Marekani awali alikaririwa akisema kuwa Shiwen ambaye alivunja rekodi katika mashindano ya uogeleaji ya mita 400 alikuwa ametumia kitu cha ziada kutokana na kasi aliyoionyesha katika mzunguko wa mwisho uliopelekea kuvunja rekodi hiyo. Kwa upande mwingine polisi jijini London walimkamata kijana mmoja kutokana na tuhuma za kutuma ujumbe wa kuudhi katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii twitter kwenda kwa mpiga mbizi wa Uingereza Tom Daley. Kikosi cha timu taifa ya Uingereza kinatarajiwa kutupa karata yake ya kwanza baadae leo kuwania medali katika michezo ya canoeing, sarakasi, kupiga mbizi, na kukimbiza farasi.

No comments:

Post a Comment