Wednesday, August 1, 2012

SHEWEN ANYAKUWA DHAHABU NYINGINE.

Yen Shuwen.
MUOGELEAJI kinda kutoka China Yen Shiwen ameshinda medali yake ya pili ya dhahabu ya mita 200 katika michuano ya kuogelea ya Olimpiki inayoendelea jijini London. Shiwen mwenye umri wa miaka 16 ambaye alishinda medali ya dhahabu pia katika mashindano hayo ya mita 400 kwa kutumia muda wa dakika 7.57 na kuweka rekodi ya muda wa kasi zaidi katika michuano hiyo. Katika mashindano hayo Alicia Coutts alishika nafasi ya pili na kupewa medali ya fedha akitumia muda wa dakika 2.08.15 wakati Caitlin Leverenz wa Marekani alishinka nafasi ya tatu na kupata medali ya shaba akitumia muda wa dakika 2.08.95. Katika michuano hiyo China inaongoza kwa kunyakuwa medali nyingi zaidi ikiwa imejikusanyia medali 23, dhahabu 13 fedha sita na shaba nne, nchi inayofuatia ni Marekani nayo ikiwa na idadi sawa ya medali 23 lakini wenyewe wakiwa na dhahabu tisa fedha nane na shaba sita. Nchi ya tatu kwa wingi wa medali mpaka sasa ni Ufaransa ambayo imenyakuwa medali 11, medali nne za dhahabu, tatu za fedha na nne za shaba.

No comments:

Post a Comment