Wednesday, November 28, 2012

HIDDINK KUSTAAFU MWISHONI MWA MSIMU.

MENEJA wa klabu ya Anzhi Makhachkala, Guus Hiddink amesema kuwa anatarajia kustaafu kufundisha soka mwishoni mwa msimu huu. Hiddink amewahi kuziongoza timu za taifa za Uholanzi na Korea Kusini katika nusu fainali ya michuano ya Kombe la Dunia na pia kuifikisha Urusi nusu fainali ya michuano ya Kombe la Ulaya pamoja na kushinda Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na klabu ya PSV Eindhoven ya Uholanzi. Kocha huyo ambaye mkataba wake na klabu ya Anzhi unaishia katikati ya mwaka 2013 amesema kuwa bado anajiona ana nguvu za kuendelea kufundisha lakini inabidi awe mwangalifu asifundishe kwa muda mrefu. Hiddink mwenye umri wa miaka 66 ambaye amewahi kuzifundisha pia klabu za Real Madrid na Chelsea amekiri kuwa kama akifanikiwa kuiwezesha Anzhi kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa mwakani anaweza kubakia hapo kwa mwaka mmoja zaidi.

No comments:

Post a Comment