Wednesday, January 30, 2013

OBI MIKEL ATAMBA NIGERIA KUCHUKUA AFCON.

KIUNGO nyota wa kimataifa wa Nigeria, John Obi Mikel amedai kuwa timu yake ya taifa itaibuka kidedea katika michuano ya Mataifa ya Afrika inayoendelea nchini Afrika Kusini baada ya kutinga hatua ya robo fainali. Nigeria ilifanikiwa kutinga hatua hiyo jana baada ya kuibugiza Ethiopia kwa mabao 2-0 na sasa wanakabiliwa na mchezo dhidi ya Ivory Coast ambao wanapewa nafasi kubwa ya kutwaa taji la michuano hiyo kutokana nyota wake waliosheheni kwenye kikosi chake. Obi Mikel amesema kutokana na kiwango cha hali walichocheza katika mchezo dhidi ya Ethiopia ana imani kuwa wanaweza kuvuka kikwazo kilichopo mbele yao kama wakiendeleza juhudi zilezile. Nigeria imemaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi C ambalo linaongozwa na Burkina Faso.

No comments:

Post a Comment