Thursday, February 28, 2013

UEFA YAMUWASHIA TAA YA KIJANI DROGBA.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Ivory Coast, Didier Drogba ameruhusiwa kuendelea kuichezea klabu ya Galatasaray katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya Shirikisho la Soka la bara hilo-UEFA kutupilia mbali madai ya klabu ya Schalke 04 ya Ujerumani. Drogba mwenye umri wa miaka 34 alicheza mchezo wake wa kwanza akiwa na Galatasaray katika michuano hiyo ya Ulaya dhidi ya Schalke Februari 20 katika hatua ya timu 16 bora ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1. Baada ya mchezo huo klabu ya Schalke ilipeleka malalamiko yake UEFA ikidai kuwa nyota huyo wa zamani wa UEFA hakusajiliwa kwa wakati ambao ungemuwezesha kucheza mechi za michuano hiyo. Hata hivyo UEFA ilitupilia mbali madai hayo ambapo kama Galatasaray wangekutwa na hatia ya kuchezesha mchezaji huyo kinyume cha sheria Schalke wangepewa ushindi wa mabao 3-0. Drogba amesajiliwa na Galatasaray kwa mkataba wa miezi 18 akitokea klabu ya Shanghai Shenhua ya China. 

No comments:

Post a Comment