
Monday, April 1, 2013
BERCELONA HAWATUTISHI - MOURA.
MCHEZAJI nyota wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG ya Ufaransa, Lukas Moura ana matumaini makubwa ya kikosi chake kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa kwa kuing’oa Barcelona, akisisitiza kuwa wapinzani wao hao sio bora kama watu wengi wanavyosema. Barcelona ni mojawapo ya timu zinazopewa nafasi kubwa ya kunyakuwa taji la michuano hiyo ya Ulaya msimu huu lakini Moura ambaye ni raia wa Brazil anaamini kuwa timu hiyo ina udhaifu mkubwa ambao watautumia wakati watakapokutana kesho. Moura amesema amekisifu kikosi cha Barcelona kwa kusheheni nyota wakali na kucheza soka la kuvutia duniani lakini hana shaka kwamba kocha wao Carlo Ancelotti atawapa mbinu kabambe ili kuhakikisha wanatumia vyema udhaifu wa wapinzani wao ili kuhakikisha wanaibuka kidedea. Nyota huyo ambaye alikuwa akicheza klabu ya Santos kabla ya kutua PSG pia amedai kumhusudu nyota wa zamani wa klabu hiyo na Barcelona Ronaldinho na ana matumaini ya kufuata nyayo zake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment