
Tuesday, April 2, 2013
RONALDO AMHIMIZA NEYMAR KUTIMKIA ULAYA.
MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Ronaldo de Lima amemtaka nyota anayechipukia wa nchi hiyo Neymar kuangalia uwezekano wa kutafuta klabu Ulaya ili kuongeza uzoefu zaidi kabla ya michuano ya Kombe la Dunia 2014. Neymar mwenye umri wa miaka 21 ambaye kwasasa amekuwa anacheza katika klabu ya Santos amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhitajika katika klabu za Bayern Munich ya Ujerumani na Barcelonaya Hispania lakini mwenyewe amekuwa akisisitiza kubakia nchini kwake mpaka mkataba wake utakapomalizika 2014. Ronaldo amesema hakuna shaka kwamba Neymar ni mzuri na atakuwa mmoja wa wachezaji bora duniani wakati atakapoamua kucheza soka Ulaya kwani ana kipaji cha hali ya juu. Nguli huyo mwenye umri wa miaka 36 amedai kuwa muda mzuri wa Neymar kwenda Ulaya ni kabla ya michuano ya Kombe la Dunia 2014 kwani itamsaidia kukomaa kiuchezaji na kupata uzoefu zaidi wa kuingoza Brazil.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment