Friday, April 26, 2013

SUAREZ AMEJITAKIA - WENGER.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa adhabu ya kufungiwa mechi 10 aliyopewa mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez ni matokeo ya tabia zake kipindi cha nyuma. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay amekubali adhabu ya kufungiwa mechi tatu kwa tukio alilofanya na amepewa siku moja kukata rufani dhidi ya adhabu ya mechi saba zaidi zilizoongezwa. Wenger amesema anaamini tabia za nyota huyo kipindi cha nyuma ndio zimepelekea kupewa adhabu za mara kwa mara hivyo hana wa kumlaumu zaidi ya yeye mwenyewe. Suarez amekuwa akiingia matatani mara kwa mara kutokana na tabia zake za kushindwa kudhibiti hasira zake ambapo aliwahi kufungiwa mechi saba wakati akiwa katika klabu ya Ajax Amsterdam kwa kumng’ata kiungo wa PSV Eindhoven Otman Bakkal kwenye bega Novemba mwaka 2010. Mbali na tukio hilo nyota huyo ambaye alinunuliwa na Liverpool kwa paundi milioni 23 alifungiwa mechi nane na kutozwa faini ya paundi 40,000 na Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa kumfanyia vitendo vya kibaguzi beki wa Manchester United Patrice Evra.

No comments:

Post a Comment