Monday, May 27, 2013

MARCEDES KUFANYIWA UCHUNGUZI NA FIA WAKITUHUMIWA KUFANYA MAJARIBIO YA KIUFUNDI KINYUME CHA UTARATIBU.

TIMU ya Marcedes inakabiliwa na uchunguzi kutoka kwa chama kinachosimamia mbio za magari yaendayo kasi ya langalanga-FIA baada ya kutuhumiwa kujaribu matairi yao kinyume cha utaratibu. Timu za Red Bull na Ferrari zilipelekea malalamiko hayo katika michuano ya Monaco Grand Prix baada ya kugundua matairi yanayotengenezwa na kampuni ya Pirelli yanayotumiwa na Mercedes yalifanyiwa majaribio kwa siku tatu. Kwenye sheria za mashindano hayo msimu ukishaanza majaribio huwa hayaruhusiwi labda kwa madereva chipukizi au kwa kiwango kilichowekwa ambacho ni kilometa 1,000 lakini Pirelli wamedai kuwa wana mkataba na FIA unaowaruhusu kufanya majaribio kwa kiwango. Hata hivyo Red Bull na Ferrari wamedai kuwa sheria inasema kama utafanya majaribio kwa kiwango hicho kilichowekwa inabidi utumie aina ya gari ambalo limeshatumika kwa zaidi ya miaka miwili lakini Marcedes wao walitumia gari lao jipya lilitoka 2013 pamoja na madereva wao nyota Lewis Hamilton na Nico Rosberg. Timu pinzani na Marcedes zimefikia hatua kwasababu majaribio kama hayo ya ziada yanaweza kuwapa faida ya kiufundi hivyo kuwawezesha kufanya vizuri zaidi.

No comments:

Post a Comment