Sunday, May 26, 2013

SUALA LA KUONDOKA KWANGU HALIHUSIANI NA MASUALA YA FEDHA - ANCELOTTI.

MENEJA wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG, Carlo Ancelotti amesisitiza kuwa ombi lake la kuondoka klabuni hapo ni suala la binafsi na halihusiani na mambo ya kifedha. Akiongea kabla ya mechi ya mwisho ya Ligi Kuu nchini Ufaransa maarufu kama Ligue 1 dhidi ya Lorient, Ancelotti aliongeza kuwa hajazungumza na klabu yoyote toka aweke wazi kutaka kwake kuondoka mwishoni mwa wiki iliyopita. Kocha huyo aliendelea kusema kuwa uamuzi wa kutaka kuondoka ni wa binafsi zaidi na hauhusiani na mtu au kiongozi yoyote ndani ya klabu hiyo na pia siyo suala la fedha. Anceloti Jumapili iliyopita alibainisha kuwa kuna uwezekano akaelekea kuifundisha klabu ya Real Madrid baada ya Jose Mourinho kutangazwa kuondoka mwishoni mwa msimu lakini klabu hiyo imeonekana haitaki kumuachia kocha huyo. Hata hivyo Ancelotti amesisitiza kuwa hakuna chochote kilichoongelewa kwa wiki hii na mambo yote yapo kama yalivyozungumzwa wiki iliyopita.

No comments:

Post a Comment