Tuesday, July 30, 2013

AL MASRY WAONDOLEWA ADHABU YA KUFUNGIWA.

CHAMA cha Soka nchini Misri-EFA kimetangaza kuiondolea adhabu timu ya Al Masry kwa kuiruhusu kushiriki msimu mpya wa Ligi Kuu nchini humo ambayo inatarajiwa kuanza Agosti 22 mwaka huu. Al Masry walifungiwa mwaka mmoja na EFA baada ya vurugu zilizotokea Port Saied Februari mwaka jana ambapo mashabiki zaidi ya 72 wa Al Ahly waliuawa uwanjani. Msemaji wa EFA Azmy Megahed amesema Mahakama ya Usuluhishi wa Miechezo ya CAS imeiruhusu Al Masry kucheza na tayari wameshalipa ada yao ya ushiriki katika ligi hiyo. Hata hivyo Al Masry watakabiliwa na tatizo la kutafuta uwanja mwingine wa kutumia katika mechi zao za nyumbani kutokana na adhabu ya kufungiwa miaka mitatu uwanja wao wa Port Saied ikiwa bado haijamalizika. Maofisa awa Al Masry wanataka mechi zao kuchezwa Al Ismailiya lakini majeshi ya ulinzi walikataa wazo hilo kwasababu za kiusalama.

No comments:

Post a Comment