Monday, July 22, 2013

MOURINHO AMTAKA MOYES KUACHANA NA NDOTO ZA KUMREJESHA RONALDO OLD TRAFORD.

MENEJA mpya wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amempasha meneja wa Manchester United, David Moyes kusahau ndoto zake za kujaribu kumrejesha Cristiano Ronaldo Old Traford. Kuna tetesi kuwa United wako katika harakati za kujaribu kumrejesha nyota huyo wa kimataifa wa Ureno pamoja na meneja mpya wa Real Madrid Carlo Ancelotti kusisitiza kuwa hawatamuuza. Lakini Mourinho ambaye msimu uliopita alikuwa akiinoa klabu hiyo amedai kuwa hadhani kama Madrid wanaweza kumruhusu Ronaldo kuondoka kwasababu ya uwezo mkubwa wa kifedha walionao kwasasa. Mourinho amesema Madrid ni klabu tajiri duniani na hawana sababu ya kumuuza nyota huyo hivyo wanaweza kukataa ofa yoyote itakayotolewa kwa ajili ya kumchukua.

No comments:

Post a Comment