Tuesday, July 30, 2013

NITAITUMIKIA DORTMUND KWA NGUVU ZANGU ZOTE PAMOJA NA YALIYOTOKEA - LEWANDOWSKI.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Borussia Dortmund, Robert Lewandowski ameahidi dhamiri yake ya kujitoa kwa dhati kwa klabu hiyo pamoja na kushindikana kwa uhamisho wake kwenda klabu ya Bayern Munich katika kipindi cha usajili wa majira ya kiangazi. Lewandowski ambaye mkataba wake na Dortmund unamalizika 2014 alikataa kusaini mkataba mpya msimu uliopita akidai kuwa anategemea kuchagua klabu atakayokwenda mapema. Baada ya usajili kuanza na Lewandowski kutaka kuwa mchezaji wa pili kuchukuliwa na mahasimu wao Bayern baada ya Mario Goetze, Dortmund walizuia uhamisho wa nyota huyo ambao ungewaletea mamilioni ya euro. Lewandowski alikaririwa na gazeti moja nchini Ujerumani akidai kuwa atajitoa kwa nguvu zake zote kwa Dortmund haijalishi kitu gani kimetokea kwani aanapokuwa uwanjani huwa hafikirii mambo hayo. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Poland alimaliza msimu uliopita vyema kwa kufunga mabao 24 katika Ligi Kuu nchini Ujerumani na kuongeza mengine 10 katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya yakiwemo mabao manne aliyofunga katika mchezo mmoja dhdi ya Real Madrid.

No comments:

Post a Comment