Wednesday, July 24, 2013

SIJUTII KUINUNUA QPR - FERNANDES.

MMILIKI wa klabu ya Queens Park Rangers, QPR, Tony Fernandes amesema hajutii kuinunua klabu hiyo pamoja na kushuka daraja na kudai kuwa ana mategemeo ya kuigeuza na kuwa klabu yenye mafanikio. Fernandes ambaye alitenga mamilioni ya paundi kwa ajili ya kuibakisha klabu hiyo ligi kuu amesema hana mpango wa kumiliki klabu kubwa kama Liverpool au Arsenal kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kununua mafanikio ya wengine. Bilionea huyo wa Malaysia ameamua kuchagua QPR ili aweze kuipa mafanikio kama zilivyo klabu nyingine kubwa nchini Uingereza na ana mategemeo ya kurejea tena ligi kuu katika kipindi cha muda mfupi ujao. Fernandes ambaye pia anamiliki timu ya Caterham ya langalanga amesema alikuwa akijua kuwa kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kushuka daraja wakati alipoinunua klabu hiyo mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment