Friday, August 30, 2013

ARSENAL YAPANGWA KUNDI LA KIFO CHAMPIONS LEAGUE.

KLABU ya Arsenal huenda ikakabiliwa na kibarua kigumu katika mechi za kutafuta nafasi ya kuingia hatua ya mtoano ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Katika mechi za makundi ya michuano hiyo Arsenal imepangwa kundi moja na timu za Borussia Dortmund ya Ujerumani, Olympique Marseille ya Ufaransa na Napoli ya Italia. Arsenal ilifuzu hatua ya makundi baada ya kuifunga Fenerbahce ya Uturuki kwa jumla ya mabao 5-0 katika mechi za mikondo miwili. Timu nyingine ya Uingereza itakayo kuwa na wakati mgumu katika mechi hizo za makundi ni Celtic ya Scotland kwani imepangwa kucheza na wababe wa soka Barcelona, AC Milan ya Italy na Ajax ya Uholanzi. Manchester City wao wamepangwa kundi moja na timu za Bayern Munich ya Ujerumani ambao ni mabingwa watetezi wa michuano hiyo, CSKA Moscow na Viktoria Plzen huku mahasimu wao Manchester United wakipangwa na Shakhtar Donetskya Ukraine, Bayer Leverkusen ya Ujerumani na Real Sociedad ya Hispania. Chelsea wenyewe wamepata kundi jepesi miongoni mwa timu za Uingereza ambapo watachuana na timu za Schalke ya ujerumani, FC Basel na Steaua Bucharest.

No comments:

Post a Comment