Friday, August 30, 2013

NADAL AZIDI KUCHANJA MBUGA US OPEN.

MCHEZAJI nyota wa tenisi, Rafael Nadal ameendeleza ubabe katika michuano ya wazi ya Marekani kwa kumgaragaza Rogerio Dutra Silva wa Brazil na kutinga mzunguko wa tatu wa michuano hiyo inayofanyika jijini New York. Nadal anayeshika namba mbili katika orodha za ubora duniani kwa upande wanaume alifanikiwa kumfunga Dutra Silva kwa 6-2 6-1 6-0 kwa kutumia dakika 92 pekee. Kwa upande mwingine bingwa mtetezi kwa upande wa wanawake Serena Williams, bingwa mara tano wa michuano hiyo Roger Federer na Victoria Azarenka wote walifanikiwa kutinga mzunguko wa tatu wa michuano hiyo baada ya kushinda mechi zao. Williams alitinga hatu hiyo baada ya kumfunga Galina Voskoboeva kwa 6-3 6-0 wakati Federer alisonga mbele baada ya kumfunga Carlos Berlocq 6-3 6-2 6-1 huku Azarenka akimgaragaza Aleksandra Wozniak kwa 6-3 6-1.

No comments:

Post a Comment