Sunday, August 25, 2013

TYSON AKIRI KUZIDIWA NA MADAWA NA POMBE.

BINGWA wa zamani wa ngumi za uzito wa juu, Mike Tyson wa Marekani amedai kuwa anakaribia kufa kutokana na matatizo ya kutumia madawa na pombe nyingi. Tyson mwenye umri wa miaka 47 alikiri kuwa amekuwa akinywa pombe kupita kiasi lakini ana mategemeo ya hali yake kutengemaa baada ya kuanza matibabu. Akihojiwa na luninga ya ESPN, Tyson amesema anataka kuishi maisha ya bila kutumia kilevi chochote kwasababu hataki kufa. Mwaka 1987 akiwa na umri wa miaka 20 Tyson aliweka rekodi ya kuwa bingwa wa ngumi mdogo zaidi kushikilia mikanda ya uzito wa juu ya WBC, WBA na IBF. Lakini miaka mitano baadae Tyson alikamatwa kwa kosa la kumbaka mrembo Desiree Washington na kufungwa miaka sita jela na baadae kurejea tena ulingoni lakini aliamua kustaafu mwaka 2006 na sasa anafanya shughuli za upromota.

No comments:

Post a Comment