Wednesday, February 19, 2014

MIMI NI MGONJWA NA SIO CHAPOMBE - WILKINS.

KOCHA msaidizi Ray Wilkins aliyetimuliwa kibarua chake na Fulham mapema wiki hii amebainisha kuwa anasumbuliwa na ugonjwa kama uliokuwa ukimsumbua kiungo wa Manchester United Darren Fletcher. Wilkins mwenye umri wa miaka 57 ambaye amewahi kucheza katika timu za United na Chelsea amekuwa akipambana na ugonjwa wa vidonda vya tumbo toka mwaka 1990. Wilkins amelazimika kuweka wazi hali yake ya kiafya ili kuokoa kibarua chake kama mwalimu wa soka na kuzima tuhuma kuwa ni mlevi. Akihojiwa kocha huyo amesema amesikia tuhuma kuwa alionekana amelewa wakati wa mchezo dhidi ya Liverpool ambao walichapwa mabao 3-2 na kupelekea benchi zima la ufundi la timu hiyo likiongozwa na kocha mkuu Rene Meulensteen kutimuliwa. Wilkins alikana tuhuma hizo na kubainisha kuwa hali yake ya kiafya muda mwingine humfanya aonekane katika hali hiyo.

No comments:

Post a Comment