MAWAKILI wa mwanariadha nyota wa Afrika Kusini Oscar Pistorius wameanza tena kumhoji shahidi muhimu. Kesi ya Pistorius ilianza hapo jana katika makahama iliyopo jijini Pretoria. Jana shahidi mmoja wa upande wa waendesha mashtaka, Michelle Burger ambaye ni jirani wa Pistorius aliieleza mahakama kuwa alisikia kile alichokitaja kama kelele za mauaji zikitoka katika nyumba anayoishi Pistorius, zilizofuatiwa na milio ya bunduki, katika usiku ule alipomuua mpenzi wake. Mwanariadha huyo wa paralimpikic ambaye miguu yake imekatwa na hukimbia kwa kusaidiwa na miguu bandia amekana mashitaka na kudai kuwa alimpiga risasi mpenzi wake Reeva Steenkamp bila kukusudia baada ya kudhania kuwa alikuwa ni mtu alievamia nyumba yake.
No comments:
Post a Comment