Saturday, March 22, 2014

WENGER AKUBALI LAWAMA KUFUATIA KIPIGO CHA MABAO 6-0.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amekubali kubeba lawama zote kufuatia kipigo cha kudhalilisha cha mabao 6-0 ilichopata kutoka kwa mahasimu wao aktika mbio za ubingwa Chelsea. Wenger ambaye alitimiza mechi yake ya 1,000 katika mchezo huo ameeleza kuwa kama siku mbaya katika kazi yake ya ukocha baada ya kikosi chake kujikuta nyuma kwa mabao 3-0 huku wakiwa pungufu baada ya dakika 17. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Wenger amesema hilo ni kosa lake na anakubalia kubeba lawama zote kwa kiwango wachocheza hivyo hadhani kama kuna haja ya kuzungumza sana kutokana na makosa waliyofanya. Wenger amesema jambo la muhimu ni kusahau maumivu ya mechi hiyo na kuhamishia nguvu katika mchezo wa Jumanne dhidi ya Swansea City.

No comments:

Post a Comment