Friday, November 21, 2014

FIFA KUPITIA UPYA RIPOTI YA GARCIA.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limethibitisha kamati yake ya ukaguzi itapitia upya taarifa yote ya mchakato wa uenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na 2022 baada ya kikao kati ya wakili Michael Garcia na jaji wa maadili Hans-Joachim Eckert. Taarifa ya mapitio ya ripoti ya uchunguzi wa Garcia kuhusiana na masuala ya rushwa ilitolewa na jaji Eckert wiki iliyopita huku Urusi na Qatar zikisafishwa kuwa wenyeji halali wa michuano hiyo ya mwaka 2018 na 2022. Jaji Eckert alikiri kuwepo matukio kadha katika ripoti hiyo lakini hayakuingilia mchakato wa kutafuta wenyeji katika michuano hiyo. Haraka taarifa hiyo iliyokuwa na kurasa 42 ilipingwa vikali na wakili Garcia alioongoza uchunguzi huo kwa miaka miwili akisisitiza kumekuwa na makosa kadhaa kadhaa kulinganisha na ripoti yake iliyokuwa na kurasa 430. Jaji Eckert na Garcia alikutana ili kusawazisha mambo na kufikia uamuzi huo wa kupeleka ripoti yote kwa kamati ya ukaguzi kwa ajili ya kufanyiwa kazi zaidi.

No comments:

Post a Comment