Friday, January 23, 2015

BENITEZ ASISITIZA KUBAKIA NAPOLI.

MENEJA wa Napoli Rafa Benitez amesisitiza anafurahi kuwepo katika klabu hiyo na anatarajia kufanya mazungumzo kuhusiana na mustakabali mwishoni mwa msimu huu. Mkataba wa sasa kocha huyo na klabu hiyo unatarajiwa kumalizika Juni mwaka huu. Benitez amesema anatarajia kuzungumzia mustakabali wake na rais wa Napoli Aurelio De Laurentiis mwanzoni mwa kiangazi huku akidai kuwa hajafanya mazungumzo na klabu yeyote. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa anafurahi kuinoa Napoli ndio maana anataka kuendelea kubakia hapo na kuiwezesha timu hiyo kunyakuwa mataji.

No comments:

Post a Comment