Wednesday, February 18, 2015

NYOTA WA LIVERPOOL ALIMWA ADHABU YA MECHI NNE UEFA.

MCHEZAJI wa Liverpool Lazar Markovic amefungiwa mechi nne za Ulaya na Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA kwa kadi nyekundu aliyopewa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya FC Basel Desemba mwaka jana. Markovic mwenye umri wa miaka 20 alitolewa nje kwa kumpiga kofi usoni Behrang Safari katika dakika za mwisho za mchezo huo ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 na Liverpool kuenguliwa katika michuano hiyo. UEFA imeongeza mechi zaidi baada ya Markovic pia kutolewa nje akiitumikia Benfica msimu uliopita katika nusu fainali ya Europa League. Liverpool haitakata rufani kutokana na adhabu hiyo hivyo kumfanya kuukosa mchezo wa Europa League dhidi ya Besiktas kesho na kama wakifanikiwa kusonga mbele ataweza tena kuwepo katika kikosi cha timu hiyo katika hatua ya robo fainali.

No comments:

Post a Comment